Zaburi Sura 52
1
Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.
2
Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila
3
Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.
4
Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.
5
Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.
6
Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka;
7
Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake.
8
Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.
9
Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.