1 Mambo ya Nyakati Sura 25
1
Tena Daudi na maakida wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na matoazi; hii ndiyo hesabu ya wafanya kazi sawasawa na utumishi wao;
2
wa wana wa Asafu; Zakuri, na Yusufu, na Nethania, na Asharela, wana wa Asafu; walioamriwa na Asafu, aliyetabiri kwa amri ya mfalme.
3
Wa Yeduthuni; wana wa Yeduthuni; Gedalia, na Seri, na Yeshaya, na Hashabia, na Matithia, [na Shimei] , watu sita; walioamriwa na baba yao Yeduthuni mwenye kinubi, aliyetabiri katika kumshukuru na kumsifu Bwana.
4
Wa Hemani; wana wa Hemani; Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, na Yeremothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, na Romanti-ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri, Mahaziothi;
5
hao wote ndio wana wa Hemani, mwonaji wa mfalme, kwa maneno ya Mungu, ili kuinua pembe. Naye Mungu akampa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu.
6
Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa Bwana, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme.
7
Na hesabu yao, pamoja na ndugu zao waliofundishwa kumwimbia Bwana, wote waliokuwa wastadi, walikuwa mia mbili na themanini na wanane.
8
Wakatupiwa kura ya ulinzi wao, sawasawa wote, mdogo kwa mkubwa, mwalimu kwa mwanafunzi.
9
Kura ya kwanza ikamtokea Yusufu, kwa Asafu; ya pili Gedalia; yeye na nduguze na wanawe, kumi na wawili;
10
ya tatu Zakuri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
11
ya nne Seri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
12
ya tano Nethania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
13
ya sita Bukia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
14
ya saba Asharela, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
15
ya nane Yeshaya, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
16
ya kenda Matania wanawe na nduguze, kumi na wawili;
17
ya kumi Shimei, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
18
ya kumi na moja Uzieli, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
19
ya kumi na mbili Hashabia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
20
ya kumi na tatu Shebueli, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
21
ya kumi na nne Matithia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
22
ya kumi na tano Yeremothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
23
ya kumi na sita Hanania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
24
ya kumi na saba Yoshbekasha, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
25
ya kumi na nane Hanani, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
26
ya kumi na kenda Malothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
27
ya ishirini Eliatha, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
28
ya ishirini na moja Hothiri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
29
ya ishirini na mbili Gidalti, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
30
ya ishirini na tatu Mahaziothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
31
ya ishirini na nne Romanti-ezeri, wanawe na nduguze, kumi na wawili.