Skip to Content

"zimo"

10 mara katika SUV

Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo.

Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Basi nikageuka nikashuka kutoka mlimani, nikazitia mbao ndani ya sanduku nililofanya; nazo zimo humo kama alivyoniamuru Bwana.

Nyakati zangu zimo mikononi mwako; Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia.

Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; Uovu na taabu zimo ndani yake;

Tamaa mbaya zimo ndani yake; Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.

Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako, Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.

Mkononi mwake zimo bonde za dunia, Hata vilele vya milima ni vyake.

Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.

Upanga uko nje, na tauni na njaa zimo ndani; yeye aliye nje mashambani atakufa kwa upanga; na yeye aliye ndani ya mji, njaa na tauni zitamla.