Naliomba nipewe mtoto huyu; Bwana akanipa dua yangu niliyomwomba;
Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua.
Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
Akasema, Nalimlilia Bwana kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu naliomba, Nawe ukasikia sauti yangu.