Umewakemea mataifa; Na kumwangamiza mdhalimu; Umelifuta jina lao milele na milele;
Bwana amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.
Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, Naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.
Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; Bwana huwatia nuru macho yao wote wawili.
Bwana asema hivi, Fanyeni hukumu na haki, mkamtoe yeye aliyetekwa katika mikono ya mdhalimu; wala msiwatende mabaya mgeni, wala yatima, wala mjane, wala kuwadhulumu, wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia katika mahali hapa.