Skip to Content

"magamba"

10 mara katika SUV

Katika hao wote walio ndani ya maji mtakula hawa; kila aliye na mapezi na magamba, ndani ya hayo maji, na ndani ya bahari, na ndani ya mito, mtakula hao.

Na hao wote wasio na mapezi na magamba, ndani ya bahari, na ndani ya mito, katika hao waendao majini, na katika wote wenye uhai, waliomo majini, hao ni machukizo kwenu,

Kila asiye na mapezi wala magamba aliye ndani ya maji ni machukizo kwenu.

Mtakula hawa katika wote walio majini; kila kilicho na mapezi na magamba mtakula;

na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.

Ni nani awezaye kumbambua magamba yake? Ni nani atakayepenya dirii yake maradufu?

Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri.

Nami nitatia kulabu katika taya zako, nami nitawashikamanisha samaki wa mito yako na magamba yako; nami nitakutoa katika mito yako, pamoja na samaki wa mito yako walioshikamana na magamba yako.

Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.

Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa;