Labani akampa binti yake Raheli mjakazi wake Bilha, awe mjakazi wake.
Akasema, Yuko mjakazi wangu, Bilha, uingie kwake ili kwamba azae juu ya magoti yangu, nami nipate uzao kwa yeye.
Basi akampa Bilha mjakazi wake kuwa mkewe. Yakobo akaingia kwake.
Naye Bilha akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana.
Bilha, mjakazi wa Raheli, akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.
na huko Bilha, na Esemu, na Toladi;
Wana wa Naftali; Yaseeli, na Guni, na Yeseri, na Shilemu; wana wa Bilha.