Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.
Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.
Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.